Jorafra Transport Agency Ltd inatangaza nafasi za ajira kwa waombaji wenye sifa stahiki kama ifuatavyo:

1. Usajili wa Leseni za Bajaji na Pikipiki

Mkoa wa Mwanza – Nafasi 25

  • Kwimba – 5
  • Misungwi – 5
  • Sengerema – 5
  • Magu – 5
  • Buchosa – 5

Mkoa wa Dar es Salaam – Nafasi 15

2. Afisa Masoko (Marketing Officer)

Maeneo: Dar es Salaam na Arusha

Idadi: 1 kila mkoa

Mahitaji ya jinsia na umri: Kiume, miaka 22–30

Sifa za Mwombaji

  • Awe Mtanzania na mkazi wa eneo husika.
  • Ajue maeneo mengi ya mkoa husika.
  • Elimu: Diploma au zaidi katika fani husika, Business Administration, au Logistics.
  • Uzoefu wa kazi: Angalau miaka 2 katika sekta ya Logistics au Masoko.
  • Kwa waombaji wa usajili wa leseni za pikipiki na bajaji,awe na simu janja na ajue kutumia kwa matumzi ya internet.
  • Kigezo cha Elimu wa wanaosajili leseni iwe ni kuanzia kidato cha nne na kuendelea.

Maelekezo kwa Waombaji Wote

  • Waandike barua ya maombi kwa mkono kisha wa-scan bila watermark.
  • Waambatanishe:
  • Barua ya utambulisho kutoka serikali za mitaa.
  • CV (Wasifu binafsi).
  • Tuma barua zote ziandikwe kwa anuani:

Meneja Rasilimali Watu

Jorafra Transport Agency Ltd

S.L.P 735 Mwanza

Kisha zitumwe Kwa barua pepe: vacancy@jorafra.co.tz

Muda wa Maombi

  • Kuanza kupokelewa: 05/04/2026
  • Mwisho wa kupokelewa: 15/04/2026

Wito

Wote wenye nia na sifa stahiki wanakaribishwa kuwasilisha maombi yao kwa wakati.

ONYO:

Nafasi hizi ni za wazi na zinatolewa kwa mwenye sifa zilizotajwa pekee,usitoe wala kushawishi kwa pesa kupata nafasi tajwa.